Jumatatu, 17 Julai 2017

MCHORO WENYE DHAMANI KUBWA KUWAHI KUTOKEA DUNIANI

Kama wewe ni mbukuzi kama mimi hapa nadhani ushawahi kusikia au kuona (kwenye runinga) mchoro maarufu wa MONALISA mchoro wenye dhamani kubwa sana Dunia nzima ambao watu husafiri kutoka nchi mbali mbali kwenda kuuona nchini ITALY katika makumbusho ya LOUVRE ambapo unadhamani ya Dolla millioni 785 iv , ni pesa nyingi sana , na watu mbali mbali husafili kwenda Ufaransa kuuona , una ulinzi wa Hali ya juu kwani watu kadhaa walijalibu kuuiba miaka ya nyuma . Mchoro huu ndo mchoro maarufu sana kuwahi kutokea Duniani ..

HISTORIA FUPI
Mchoro wa MONALISA ulichorwa na Leonardo Da Vinci raia wa Italy aliezaliwa 15.4.1452 hukoo nchini Italy , Leonardo ni moja ya watu makini kuwahi kutokea duniani kwani ana nadhalia zake ambazo mpaka kesho zinatumiwa sana duniani , hakuwa tu mchoraji pia alikua Mwanasayansi, Mwanahisabati, Mwanamuziki, na fani nyingine mbali mbali ndo maana wahenga kama mimi tunamuona ni moja ya ma geneus kuwahi kutokea , ikumbukwe Leonardo ndo mtunzi au msimamizi wa Nadhalia ya sayansi ya kitu kupaa angani bila kushika mahali na ndo maana hufananishwa sana na watu kama Isaac Newton, Albert Einstein, Galileo Socrates n.k Uchoraji wa picha ya MONALISA ulianza mwaka 1503 mpaka 1506 , alipoukamilisha kwa kiasi kikubwa sana , mnamo mwaka huo huo alihamia Ufaransa na kuendelea na makazi yake kule , mchoro wa MONALISA haukua mchoro wa siku wiki au mwez ulichukua mda sana , kwakua Mchoraji Leonardo alikua akijihusisha na mambo mengi ilimchukua mda sana na inaaminika ndo sababu ya picha kua nzuri adi kesho kutwa kwani ilichukua mda sanaa. Mnamo tarehe 2.5.1519 umauti ulimfika Leonardo Da Vinci mchoraji wa mchoro wa MONALISA ulikua wakawaida sana ila vitu vilivyofanya mchoro huu kua special ni kutokana na mtu mwenyewe aliemchora kua special sana katika maisha ya kawaida ..

Baada ya miaka 300 baada ya kifo cha Leonardo picha ilianzakujipatia umaarufu mkubwa sana kutokana na ustadi uliokua umetumika kuichora picha ile ule upekee wa picha na uhalisia uliifanya picha ile kuonekana special sana karne ya 19 watoto wa wafalme mbali mbali duniani waliitumia picha ile km mifano ya wanawake ambao wanatamani kuwaowa .

Salai mwanafunzi wa Leonardo alitumia picha ile kujipatia kipato kwa kuionyesha sehemu mbali mbali mnamo karne ya 19 watu mbali mbali walisafiri kwenda kuiona picha iyo ilizidi kujipatia umaarufu mwaka 1963  Rais wa Marekani kwa kipindi kile John F. Kennedy aliiomba picha iyo iende marekani na ililindwa sn na kukatiwa bima ya dolla million 600 , iliwasili nchini Marekani Washingtoni DC na watu na misululu miref ilisimamwa pale watu kuishika tu na kila mtu aliishika kwa sekunde 15 tu . Mwaka 1964 nchi kama Japani na USSR ,nazo zilizidi kuipa umaarufu sana picha ile kwani ilitakiwa kuenda pia kwa nchi hizo.

UPEKEE WA PICHA

1;Ndo ilikua picha ya kwanza ya rangi kuchorwa kwakipindi kile miaka ilipo chorwa.

2; Ulikua ni mchoro mzuri wa mtu wakusadikika ambae kila mwanaume alitamani kua na Mwanamke kama yeye na wakati hakuwepo wala hakuwahi kutokea

3; Picha ya MONALISA ilimuonyesha mwanamke mzuri ila hakuwa na Nyusi wala kidani chochote ila alikua mzuri sana .

4;Mchoraji mwenyewe Leonardo Da Vinci alikua ni moja ya ma genious wachache kuwahi kutokea Duniani .

5; Ndo picha yenye dhamani kubwa Dunia nzima adi hii leo

Iliwahi kuibiwa mwaka 1856 ila waliipata 1857 na watu wengi waliona kua picha iyo inadhamani kubwa adi hii leo inaulinzi wa bullet proof ndani ya makumbusho ya Louvre Paris nchini Ufaransa  .

By FOBES

ZIFAHAMU SEHEMU 5 JIJINI MWANZA ZENYE FURSA

Maendeleo jijini mwanza yanakua kwa kasi sana katika nyanja nyingi hasa kiuchumi na kijamii , maendeleo yanakua kwa kasi sana kila kukicha kwani Mwanza ya kitambo co sawa na Mwanza ya sasa mbali na Ziwa Victoria kua n moja ya vivutio vizuri kuwahi kuwepo jijini humo pia miundombinu imezidi kuboreshwa kila siku iendayo kwa Mungu . Ukirudi miaka mitano nyuma utakubaliana na mm kua Mwanza ya sasa imebadilika sana kwa nyanja mbali mbali barabara karbia zote mjini kati zina lami  hali inayozidi kuunyanyua uchumi kwa kasi sana..

Upanuzi wa barabara mbalimbali kati kati ya jiji umezidi kupendezesha na kurahisisha usafili hali inayopelekea kukua kwa uchumi jijini hapa , upanuzi wa barabara nne makongoro mpaka Airport unazidi kunogesha maadhali ya jiji letu au upanuzi wa barabara tatu  kati ya Mlango mmoja mpaka Igoma unazidi kufanya jiji kuonekana zuri kila kukicha. Leo ndugu yenu wa damu kabsa nmeamua kuwaleetea maeneo matano (5) ambayo ni vyepesi sn kuishi hasa mtu wa kipato cha kawaida au kipato cha chini . Ifuatayo ni list ya maeneo matano mepesi kuishi jijini Mwanza, na ntaanza na no 5 mpaka 1..


5: BUHONGWA
Hii ni seemu ya wilaya Nyamagana , pia ni kituo kikuu cha daladala zitokazo mjini kwenda Buhongwa , seem hii imechangamka sana pia inafursa za kazi na kujiajili.pia , kuna soko kubwa la mazao ya chakula na wakazi wengi wa eneo hili ni watu wa kipato cha chini kuanzia (500) unapata chakula na unaishi vizur ivyo kija yoyote , unaweza kuchukua km fursa iv ili kuendeleza harakati zako town...

4:IGOMA
Uku ni Wilaya ya Nyamagana kama kilometa 11 kutoka mjini kati , kuna machinjio kubwa Mwanza nzima ipo maeneo haya pia wepesi wa upatikanaji vitu ni mkubwa sn kwani kuna adi nguo za buku buku sharti nzuri tu unapata pia kuna uwepesi wa vyakula na fursa za ajira zipo nyingi sn kwani kuna viwanda vingi sn maeneo jiran km kijereshi na mnadani , mbali na fursa zilizopo pia ndo eneo ambalo linaongoza kua na wasukuma wengi sn jijini Mwanza , pia kuna mnada wa Ng"ombe na Mbuzi hali inayofanya pazidi kua na fursa nying za ajira , Vyumba adi elfu kumi unapata so km umechoka kukaa kwa Mama ni moja ya maeneo mazur sana kwa kuanzia maisha kwani kuna wepesi wakuishi ... 

3:PASIANSI NA MABATINI
Pasiansi ipo wilaya ya Ilemela ni eneo la makutano ya Kiloleli , Airport na Mjini kati kuna mihangaiko mingi sn usiku na mchana pia ni sehemu nyepesi kuishi kwani kuna miundombinu inayowakutanisha watu pamoja pia kuna Hotel kubwa km Lenana ambayo ni nyota tano , Mabatini ni km Kilometa 2 iv kutoka mjini ni sehemu nzuri kuishi kwa kipato chakuanzia maisha pia ni sehemu nzuri kuwekeza kama una mtonyo ivi,,  maisha yanawepesi sn kwani ata elfu kumi unapata chumba , so mdau ukimchoka mama.njoo uku kwetu, Ndo maana sisi tunapaita Califonia kwani pako km blooklyne iv au Los Angels

2:KIRUMBA
Eneo lipo maeneo ya Ilemela karbu kabsa na Ziwa victoria Km 2 kutoka mjini kati mbali ya kua ndo eneo ilipo soko kubwa la samaki jijini Mwanza ila pia ndo eneo lenye Garage nyingi na Hotel nying sn Kirumba huchangamka  24/7 , yaani masaa 24 ndani ya siku 7 za wiki kwa Mwanza hili ndo eneo ambalo la kwanza kwanza kua na Hotel na Disco la kisasa kabsa maeneo kama Villa Park Resort  La kailo ni moja ya sehemu nzuri kabsa za starehe kuanzishwa jijini hapa km umefika mwanza na una weweseka pakuwekeza njoo uku panakufaaaa sn....

Namba 1 ni NYAKATO NA NYEGEZI  Nyakato ni sehemu iliyochangamka sn jijini Mwanza mishemishe za hela ni kubwa na nyingi sana kwani wingi wa watu hufanya paonekane kama mbele yaani kuna stand kubwa ya magar ya mkoani pia kuna miundombinu mizuri kwani kuna barabara ya makutano kati ya Musoma , Mjini kati na Kilimahewa , ni moja ya sehemu nzur Mwanza, Nyegezi ni moja ya sehemu zilizochagamka kuanzia watu wenyewe na fursa zilizopo kuna stand ya magari ya mkoani hali inayoiyfanya kua na fursa nyingi sn za kujiajili na kuishi hasa km ni kijana unaeanza maisha, Kama mgeni lazma uenjoy sn au hata mwenyeji .

Kama ni mgeni jijini au mwenyeji najua ukifika maeneo hayo lazma ukubakiane na mimi , yapo maeneo mengi sana ila haya ni baadhi tu ya maeneo ambayo mimi nayakubali cku zote